Jumatano, 13 Februari 2019

Shairi



WATOTO YATIMA!

Paukwa Pakawa...,
Miaka ikasonga,
Balaa kutokea,
Ndugu kumkosa,
Kipenzi chao baba,
Alowajali wana.
Ama kweli ni ya maulana!

Mabula Na limbu,
Sasa walaani mbingu,
Kwa mpango wa Mungu,
Wao Sasa Yatima,
Je, Kwanini sisi?
Ndicho kilio cha ndugu,
Kwa huzuni Na uchungu.

Kama ilivyo ada,
Kifo ndio mada,
Lakini kupita muda,
Majonzi yakakimbia,
Na maisha kwendelea,

Mjane anza tapatapa,
Mume mwingine apata,
Watoto wamkumbuka,
Wao kipenzi baba,
Kwa mateso wanopata,
Wote waazimu,
urithi wao kutaka,

Ba' wa kambo tatizo,
Kila kukicha mizozo,
Mithili ya wachuuzi Kwa soko,
Mara hii nzima ile uozo,
Baba huyu kikwazo,
Maisha yetu mateso,
Ila wimbo wake mezani,
Wanangu tuishi Kwa amani.

Jambo lilo baya,
 Sasa watoto Hali mbaya,
Ba' wa kambo haoni haya,
Mali zote zake,
Mabula Na limbu wasema haya!
Na Dua zao si mbaya,
Muda ukiwadia,
Nasi tutapoteza haya,
Kudai kilicho chetu,
Fahari ya nyumba yetu!

                   Na
Mwl. Philemon Masalu
Philemonmasalu@gmail.com.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni