Ukoko ama kweli ukoko,
U mtamu uulapo,
Kama nyama ya kiboko,
Lakini shida yake ukoko,
Ni huku kuliwa mwishoni!
Wengine ukoko waula,
Wakiwa wima,
Mithili ya wapiga kura,
Msitarini kumpitisha mgombea,
Walaji wagombana,
Ukoko chanzo cha uhasama,
Kila siku wasutana,
Mara o we wala sana!
Achia nasi tule!
Utamu wa ukoko,
Wamponza koo,
Kisu Kwa Shingo,
Pasi jasho la mbio,
Ukoko chanzo cha mapigo.
13/10/2018).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni