"OKTOBA KUMI NA NNE"
Oktoba kumi Na nne,
Siku siitamani Mie,
Hunifanya nilie,
Kila nikikumbuka,
Hayati Mwalimu!
Kipaza sauti kilipotangaza,
Sikuweza kuamini,
Baba kumpoteza,
Akili ilizizima,
Na mji vilio kutanda,
Katuacha mwalimu!
Mazishi yalipoisha,
Nia mimi nikaiweka,
Kumuenzi mwalimu,
Kwa yake Kalamu,
Iliyotufundisha ufahamu,
Hayati mwalimu!
Ndugu zangu nao nia moja,
Kwa pamoja walinia,
Mwalimu ndio msingi,
Wa kuijenga nyumba,
Lo! Kumbe Nia yao usoni,
wapishi Na wanazuoni,
Kuyajenga yao matumbo,
Hakika! Kufa kufaana,
Ndivyo wanavyosema.
Takukumbuka mwalimu!
Miaka kumi sita kujongea,
Mjomba kaingia,
Jikoni kupashikilia,
Chakula kukipakua,
Kwa usawa tupate tumia,
Kumbe wengine waumia,
Na kelele kuzipiga,
Hatuhitaji busara za marehemu,
Nyumba hii kuienedesha,
Lakini mjomba yake Nia,
Kalamu ya mwalimu kuidumisha!
Nyumba kupendeza,
Wageni kututembelea,
Kwa juhudi za mjomba,
Mimi Na wenzangu,
Heshima tumepata,
Kwa kupunguza ukata,
Na elimu nayo twapata!
Tumkumbuke mwalimu!
Kwa vyetu vyema vitendo!
Sio kuendeleza magendo,
Maana nyumba twaibomoa,
Oktoba kumi na nne,
Chachu ya kukarabati,
yetu nyumba iwe thabiti,
Tumuenzini mwalimu!
Na
Mwl. Philemon masalu
Philemonmasalu@gmail.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni