Masharti ya upachikaji wa O-rejeshi katika lugha ya Kiswahili ni pamoja Na;
*Ni lazima kuwepo na Nomino au Kiwakilishi kinachorejelewa katika mazungumzo baada ya kuwa kimetajwa wazi. Mfano: mtoto aliyeiba
*Utokeaji wa O-rejeshi mwishoni mwa kitenzi huruhusu kitenzi hicho hubeba kiambishi cha wakati .mfano pale tuchezapo
*Mara baada ya kupachika O -rejeshi katika mzizi wa "Amba" kitenzi kinachofuata hakitapata athari za moja Kwa moja za O-rejeshi.
Mfano. Mkono ambao umevunjika. Hivyo kitenzi umevunjika hakijathiriwa na kirejeshi kilichopachikwa katika mzizi -Amba-.
*Katika ngeli ya kwanza umoja (Kwa kigezo cha kisintaksia), yaani ngeli ya Yu-A/WA; O-rejeshi lazima iwe "Ye" ambayo hubeba nafasi. Mfano. Mtoto aliyepotea.
*Ni lazima kuwepo na upatanishi wa kisarufi kati ya kipashio cha urejeshi na Nomino inayorejelewa. Mfano, Kiti kilichonunuliwa kimevunjika.
Kirejeshi -cho- kinapatana na Nomino kiti.
Mwl. Masalu©2019
philemonmasalu.blogspot.com
*
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni