Alhamisi, 14 Februari 2019

DHIMA ZA Umbo la O-REJESHI ( Kiswahili kidato cha sita -Tahossa- kanda ya ziwa, 2019)

SWALI: Kwa kutumia mifano, eleza dhima tano (5) za umbo la O-rejeshi katika tungo za Kiswahili.

👉O-REJESHI ina dhima au kazi (Matumizi) zifuatazo katika tungo za Kiswahili;

✍O-rejeshi hudokeza njeo/wakati.
Mfano Juma ali-po-kwenda sisi tunaanza kula= Po  hudokeza Muda/wakati.

✍O-rejeshi hudokeza mahali(sehemu)
Mfano mahali ali-mo-lala={mo} hudokeza mahali ambapo ni ndani ya kitu
Ali-po-elekea= {Po} hudokeza mahali dhahiri.

✍O-rejeshi hudokeza namna au jinsi vitendo kilivyofanyika au mtu au kitu kilivyo.
Mfano ana-vyo- simulia (vyo)
Watoto wali-vyo- pigwa(vyo)

✍O-rejeshi hutumika kama kirejeshi, yaani kurejelea kitajwa katika umbo la kitenzi ambapo kitajwa hicho kinaweza kuwakilisha mtenda/mtendewa au mtendwa.
Mfano, Kitabu kili-cho-potea, (cho) inategemea kitabu.
Nguo zili-zo-chanika, (zo) inarejelea nguo.

✍O-rejeshi hutumika kama kiunganishi. Umbo la O-rejeshi hupachikwa katika kitenzi cha kishazi tegemezi ili kukiunga na kitenzi kikuu cha kishazi huru ambavyo kwa pamoja huunda sentensi changamano.
Mfano,
mtoto ali-ye-kuja Jana ameondoka leo. Kirejeshi ( -ye- )kinaunga vishazi viwili ambavyo ni
Mtoto alikuja Jana na Mtoto ameondoka leo.

👊Umbo la O-REJESHI hubadilika badilika kutokana na mazingira ya utokeaji au upachikwaji wake. Baadhi ya maumbo ya O-rejeshi ni pamoja Na;
 o, ye, cho, vyo, lo, po, mo, ko, zo, yo, n.k.

Mwl. Masalu©2019
Philemonmasalu.blogspot. com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni