Alhamisi, 14 Februari 2019

MAZINGIRA YA UTOKEAJI WA O-REJESHI

Swali: Kwa kuzingatia sarufi ya lugha adhimu ya Kiswahili fafanua mazingira makuu matatu ya utokeaji wa umbo la O-rejeshi.

Dhana ya O-rejeshi
*O-rejeshi ni viangama au viambishi vinavyotumika katika tungo Kwa kurejelea mawazo,nomino au maumbo yaliyokwisha tajwa au yanayojulikana, (Saluhaya,2016).

O-rejeshi ni kiambishi kinachotumiwa kurejelea kwenye nomino ambayo huwa imetajwa kabla ya kitenzi chenyewe kutajwa. Viambishi hivi husababisha utegemezi katika sentensi, (Masebo,2016).
Mfano, watoto wadogo waliocheza vizuri wamezawadiwa.

✍Mazingira ya utokeaji wa O-REJESHI

Katika lugha adhimu ya Kiswahili umbo la O-rejeshi huwezi kutokea katika sehemu kuu tatu za neno zifuatazo;

👉Katikati ya mzizi na viambishi na viambishi awali (V.A+ O-rejeshi+ mzizi wa neno)
Mfano. Iliyopotea= i-li-yo-pote-a, hapo kirejeshi "yo" kipo katikati ya viambishi awali i-, li- na mzizi -pote-

👉Mwishoni wa kitenzi (kitenzi + O-rejeshi)
Mfano liumalo= li-um-a- lo, hivyo kirejeshi -lo-kimetokea mwishoni mwa kitenzi "Uma"

👉Kwenye mzizi wa AMBA (-Amba- + O-rejeshi)
Mfano, ambacho= -Amba- +kirejeshi "cho"
Ambaye= Amba+ kirejeshi -"ye"

👌Mbali na mazingira hayo bado umbo la O-rejeshi hujitokeza katika👉 ngeli za Kiswahili,👋 japo utokeaji wake hapa hutegemea aina ya nomino inayorejelewa.
Ni dhahiri kuwa katika ngeli umbo la O-rejeshi huundwa kwa;
i. Kipatanishi cha ngeli ya nomino(kipatinishi).
ii. Mofimu {o, au ye} ya urejeshi (kirejeshi).

Mfano katika ngeli ya YU-A/WA.
Mtoto ana-ye-soma(umoja)
Watoto wana-o-soma (Wingi)

Katika ngeli ya LI/YA
Chungwa li-lilooza(Umoja)
Machungwa ya-liyooza(Wingi).

Mwl. Masalu©2019

Philemonmasalu.blogspot.com

Maoni 9 :