Swali: Kwa kuzingatia sarufi ya lugha adhimu ya Kiswahili fafanua mazingira makuu matatu ya utokeaji wa umbo la O-rejeshi.
Dhana ya O-rejeshi
*O-rejeshi ni viangama au viambishi vinavyotumika katika tungo Kwa kurejelea mawazo,nomino au maumbo yaliyokwisha tajwa au yanayojulikana, (Saluhaya,2016).
O-rejeshi ni kiambishi kinachotumiwa kurejelea kwenye nomino ambayo huwa imetajwa kabla ya kitenzi chenyewe kutajwa. Viambishi hivi husababisha utegemezi katika sentensi, (Masebo,2016).
Mfano, watoto wadogo waliocheza vizuri wamezawadiwa.
✍Mazingira ya utokeaji wa O-REJESHI
Katika lugha adhimu ya Kiswahili umbo la O-rejeshi huwezi kutokea katika sehemu kuu tatu za neno zifuatazo;
👉Katikati ya mzizi na viambishi na viambishi awali (V.A+ O-rejeshi+ mzizi wa neno)
Mfano. Iliyopotea= i-li-yo-pote-a, hapo kirejeshi "yo" kipo katikati ya viambishi awali i-, li- na mzizi -pote-
👉Mwishoni wa kitenzi (kitenzi + O-rejeshi)
Mfano liumalo= li-um-a- lo, hivyo kirejeshi -lo-kimetokea mwishoni mwa kitenzi "Uma"
👉Kwenye mzizi wa AMBA (-Amba- + O-rejeshi)
Mfano, ambacho= -Amba- +kirejeshi "cho"
Ambaye= Amba+ kirejeshi -"ye"
👌Mbali na mazingira hayo bado umbo la O-rejeshi hujitokeza katika👉 ngeli za Kiswahili,👋 japo utokeaji wake hapa hutegemea aina ya nomino inayorejelewa.
Ni dhahiri kuwa katika ngeli umbo la O-rejeshi huundwa kwa;
i. Kipatanishi cha ngeli ya nomino(kipatinishi).
ii. Mofimu {o, au ye} ya urejeshi (kirejeshi).
Mfano katika ngeli ya YU-A/WA.
Mtoto ana-ye-soma(umoja)
Watoto wana-o-soma (Wingi)
Katika ngeli ya LI/YA
Chungwa li-lilooza(Umoja)
Machungwa ya-liyooza(Wingi).
Mwl. Masalu©2019
Philemonmasalu.blogspot.com
Safi tcha ipo vzr nimekuelew kuliko nilivokua najua ...
JibuFuta.
Asanteh.
Nzrur
JibuFutaIko vizuri hii
JibuFutaAhsante
JibuFutaNmekuelewa kabisa Mungu azidi kuwa pamoja nawe asnte saana
JibuFutaAsanteni nyote mlioshiriki kutoa makini
JibuFutaAsante iko vizuri
JibuFutaNimeelewa sana asante
JibuFutanimeelew sanaaa ahsant
JibuFuta