Jumapili, 14 Novemba 2021
KAULI ZA VITENZI VYA KISWAHILI
MADA KUU: MATUMIZI YA SARUFI
MADA NDOGO: *KAULI ZA VITENZI VYA KISWAHILI*
swali: Kauli ni nini?
👊*Kauli* ni - uhusiano uliopo baina ya kitenzi na kiima au kitenzi, kiima na shamirisho.
au
👊*Kauli* -ni umbo la kitenzi linaloonesha uhusiano baina ya kiima na shamirisho.
👉Kauli za kiswahili huzalishwa na mnyambuliko wa vitenzi vya kiswahili ambao hupambanua:
+tendo la mtu anayetenda/anayefanya
+tendo la mtu anayetendwa/anayefanywa
+tendo la mtu anayetendewa/anayefanyiwa
+tendo liwezalo kutendeka/Kufanyika
+tendo la mtu atendeshwaye/afanyishwaye n.k
👉Kauli za vitenzi vya kiswahili huwa na viambishi vijenzi (Vya mnyumbuliko) vyake maalumu kutokana na kanuni maalumu.
*Kauli za kiswahili na ufafanuzi wake*
✍ *Kauli ya kutenda*
👉 Kauli hii hueleza tendo au Jambo ambalo mtendaji analitenda, amelitenda, alilitenda au atalitenda.
👉Katika Kauli hii kiima huwa na uamilifu wa kutenda.
👉Vitenzi vya Kauli hii huwa na *kiambishi tamati (alomofu ya Kauli) -"a*" baada ya mzizi hasa Kwa vitenzi vya asili ya kibantu.
Mfano, Anachek-a, alisom-a, amelal-a n.k
👉Kwa vitenzi vyote visivyo na asili ya kibantu (aghalabu vya mkopo) mzizi wa kitenzi huwa katika Kauli ya kutenda pia
mfano, anasali, atasamehe, atawaarifu, wameabudu, n.k
✍ *Kauli ya Kutendwa*
👉Ni Kauli ionyeshayo kiima au kitu au mtu fulani ni mwathirika au mpokeaji wa tendo fulani.
👉Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi wa kitenzi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu a,e,i,o au u 👉Kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-W-"*
mfano, pak-w-a, Chek-w-a, lim-w-a, som-w-a
B: Ikiwa mzizi wa kitenzi unaishia na irabu a,i, au u 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Liw-"*
mfano, Fagi-liw-a, chuku-liw-a, ti-liw-a
C: Ikiwa mzizi wa kitenzi unaishia na irabu e na o 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Lew-"*
mfano, tobo-lew-a, Bomo-lew-a, le-lew-a, poke -Lew-a.
✍ *Kauli ya Kutendea*
👉 Kauli hii huonesha kuwa mtendaji anatenda Kwa niaba, manufaa au faida ya mtu mwingine.
👉 Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu a,i na u 👉kiambishi cha Kutendea huwa *"-i-"*
mfano, pig-i-a, pak-i-a, vunj-i-a. n.k
B: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu e na o 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-e-"*
mfano, som-e-a, sem-e-a, omb-e-a n.k
C: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na na umejengwa na irabu e na o 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Le-"*
mfano, to-le-a, tembe-le-a, bomo-le-a n.k
D: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu a,i, na u 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-li-"*
mfano, ti-li-a, vu-li-a, va-li-a n.k
✍ *Kauli ya Kutendewa*
👉Kauli hii huonesha kuwa kiima au mtu fulani ananufaika na tendo lifanywalo na mtu mwingine.
👉Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu a, i,nau 👉Kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-iw-"*
mfano, pak-iw-a, pik-iw-a, ruk-iw-a, n.k
B: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu e na o 👉Kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-ew-"*
mfano, som-ew-a, sem-ew-a, n.k
C: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu e au o 👉Kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Lew-"*
mfano, zo -Lew-a, tembe-lew-a n.k
D: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu a,i au u 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Liw-"*
mfano, va-liw-a, ti-liw-a, vu-liw-a n.k
✍ *Kauli ya Kutendeka*
👉Kauli hii huonesha Hali ya Kutendeka au Kufanyika Kwa tendo fulani.
👉Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu a,i au u 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-ik-"*
mfano, pak-ik-a, pit-ik-a, ruk-ik-a, n.k
B: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu e au u 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-ek-"*
mfano, som-ek-a, chez-ek-a, n.k
C: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu e au o 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-lek-"*
mfano, zo-lek-a, tembe-lek-a, n.k
D: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu a,i au u 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Lik-"*
mfano ti-lik-a, va-lik-a, vu-lik-a. n.k
✍ *Kauli ya Kutendana*
👉Kauli hii huonesha kuwa mtu fulani anamtenda mtu mwingine na mtu mwingine anamtenda mtu huyo.
👉Kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-an-"*
mfano, pend-an-a, sem-an-a, vu-an-a, ti-an-a, zo-an-a, ruk-an-a, suk-an-a, pik-an-a n.k
✍ Kauli ya Kutendeana*
👉Kauli hii ni muunganiko wa Kauli mbili(kauli ya kutendea na kutendana).
👉Kauli hii huonesha kuwa mtu fulani anatenda Kwa niaba,faida au hasara ya mtu mwingine na Yule mwingine anatenda hivyo hivyo.
👉Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu a,i au u 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-ian-"*
mfano, pig-ian-a, pak-ian-a, ruk-ian-a n.k
B: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti na umejengwa na irabu e au o 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-ean-"*
mfano, Chez-ean-a, som-ean- a, ot-ean-a, n.k
C: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu e au o 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Lean-"*
mfano, zo-lean-a, tembe-lean-a, to-lean-a, n.k
D: Ikiwa mzizi unaishia na irabu na umejengwa na irabu a,i,au u 👉 kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-Lian-"*
mfano, va-lian-a, ti-lian-a, vu-lian-a. n.k
✍ *Kauli ya Kutendesha/Usababishi*
👉Kauli hii huonesha kuwa mtu fulani anasababisha kufanyika Kwa kitendo fulani Kwa mtu mwingine.
👉Kauli hii huwa na viambishi vijenzi vingi sana kama vile -ish-, -esh-, -lish- , -lesh-, -z-, -sh-, -iz-, -ez-, Liz, lez, -ny-, fy, vy, s.
mfano, som-esh-a, chez-esh-a, imb-ish-a, va-lish-a, zo-lesh-a, to-lez-a, ko-lez-a, tok-ez-a, pend-ez-a, zoe-z-a, lege-z-a, chem-sh-a, ogo-fy-a, po-ny-a, Taka-s-a, To-s-a. n.k
✍ *Kauli ya Kutendua*
👉Kauli hii huonesha kuwa kinyume cha tendo fulani kimetendwa.
👉Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi unaishia na irabu au konsonanti na umejengwa na irabu a,e,i,au u 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-U-"*
mfano, Teg-u-a, pang-u-a, kunj-u-a fich-u-a,fung-U-a.
B: Ikiwa mzizi unaishia na irabu au konsonanti na umejengwa na irabu O 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-O-"*
mfano, Chom-o-a, n.k
✍ *Kauli ya Kutendata*
👉Kauli hii huonesha tendo la kufanya watu au vitu kushikana au kushikamanishwa.
👉Viambishi vijenzi Vya Kauli hii huwa kama ifuatavyo:
A: Ikiwa mzizi unaishia na konsonanti 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-at-"*
mfano, Fumb-at-a, kumb-at-a , pak-at-a,
B: Ikiwa mzizi unaishia na irabu 👉kiambishi kijenzi cha Kauli hii huwa *"-t-"*
mfano, oko-t-a, koko-t-a, n.k
👊 *Kauli Nyingine ni pamoja na*:
✍+ Kauli ya Kutenduka mf. Zib-uk-a
✍+ Kauli ya kutendama mf,Fich-am-a
✍+ Kauli ya kutendeshwa mf,som-esh-w-a, chez-esh-w-a.
✍+ Kauli ya Kutendeshea. mf, pig-ish-i-a, sem-esh-e-a,
✍+ Kauli ya kutendeshewa. mf, za-lish-iw-a, chez-esh-ew-a.
✍+ Kauli ya Kutendesheana. mf, pig-ish-ian-a, chez-esh-ean-a.
✍+ Kauli ya Kutendesheka. mf, Som-esh-ek-a, ig-iz-ik-a, chem-sh-ik-a.
👌 Kwa upande wa vitenzi vyote visivyo na asili ya kibantu Kanuni za utokeaji wa viambishi vijenzi Vya Kauli huwa hazizingatiwi sana .
💬Nukuu hizi zimeandaliwa na:
🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓🎓
*MWL MASALU - IDARA YA KISWAHILI- SENGEREMA TRC OPEN SCHOOL - 14/11/ 2021*
Mawasiliano:
👂philemonmasalu@gmail.com
👂0625506120/0689897806
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Kiswahili tunu yetu
JibuFuta