Alhamisi, 12 Desemba 2019

VIPENGELE MUHIMU KATIKA USANIFU WA MAANDISHI

USANIFU WA MAANDISHI:

🎓Usanifu wa maandishi katika fasihi ni kitendo au mchakato wa kuchambua mbinu mbalimbali za kifani/kisanaa zilizotumiwa na msanii katika kuiumba kazi yake ya fasihi.

Katika fasihi, usanifu wa maandishi huhusisha matini za aina tatu:

1.Riwaya/monolojia/masimulizi.
2. Tamthiliya/dayalojia/majibizano.
3. Ushairi (mashairi na tenzi).

🎓Mbinu za kisanaa/kifani zinazochambuliwa katika usanifu wa maandishi ni pamoja na:

A. Muundo:

👉Muundo ni mpangilio au mtiririko wa visa na matukio katika kazi ya fasihi .
👊Ikiwa matini ni Tamthiliya au riwaya , muundo waweza kuwa wa;
*moja Kwa moja (msago).
*muundo rukia/rejeshi/kioo.

✊Ikiwa matini ni Shairi, muundo hubainishwa Kwa kuangalia idadi ya mishororo(Mistari) katika beti zinazounda shairi hilo.

 Miundo katika shairi ni kama ifuatavyo:

#Tamolitha/Monolitha- muundo wa shairi ambapo ubeti hujengwa na msitari mmoja tu.
#Tathnia- Mistari miwili katika ubeti
#Tathlitha- Mistari mitatu katika ubeti
#,Tarbia- Mistari minne katika ubeti
#Takhmisa- Mistari mitano katika ubeti
#Sabilia - Mistari sita na kuendelea katika ubeti.


B:Mtindo:
👉Ni namna au jinsi msanii anavyoiumba kazi yake ili kuipa upekee kati yake na wasanii wengine. Mtindo huhusisha Matumizi ya mbinu mbalimbali katika uandishi wa kazi za fasihi kama vile:
@Matumizi ya Taarifa ya habari.
@Matumizi ya matangazo.
@Matumizi ya mabango.
@Matumizi ya Nafsi
@ Matumizi ya Barua n.k

✊Ikiwa matini ni Shairi , mtindo hubainishwa Kwa kuangalia iwapo shairi linazingatia urari wa vina na mizani (mtindo wa kimapokeo) au iwapo shairi halijazingatia urari wa vina na mizani( Mtindo wa kisasa).

C . Matumizi ya Lugha .
👉  Usanifu wa maandishi huhusisha uchambuzi wa vipengele vikuu vitatu vya lugha, ambavyo ni:

#Tamathali za semi
#Semi mabalimbali.
#Mbinu nyingine za kisanaa.

-Vipengele hivi ndivyo huifanya lugha kuonekana nyepesi au ngumu katika matini hiyo.

D. Wahusika.
👉Katika katika za fasihi wahusika waweza kuainishwa Kwa vigezo vifuatavyo:

 I: Kigezo cha Uhusika wa mhusika.
- Kwa kuzingatia kigezo hiki, kuna aina kuu mbili za wahusika:
(a). Wahusika wakuu
(b). Wahusika wadogo - Hawa wanaweza kuwa wasaidizi au wajenzi.

II: Kigezo cha Sifa /Tabia za mhusika.
- Kwa kuzingatia kigezo hiki ,kuna aina tatu za wahusika:
(a). Wahusika Duara
(b). Wahusika bapa
(c). Wahusika shinda/Foili.

✊Katika usanifu wa maandishi ni muhimu kubainisha wahusika na Uhusika wao katika matini husika.


E: Mandhari.

👉 Ni sehemu au mazingira ambamo matukio na matendo katika kazi ya fasihi hutendea au hutukia. Katika fasihi Mandhari yaweza kuwa halisi au ya kubuni.
- Ni muhimu kubainisha Mandhari katika matini husika .


🎓Mwl. Philemon Benard Masalu🎓








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni